Friday, June 1, 2012

cheka

A pastor married a jealous woman. One day the woman was in the
kitchen cooking when she overheard him praying in the living room,
“Thank you Lord for bringing mercy, joy and grace into my life.” She
... ran quickly with a frying pan, whacked him on the head and said, “I
knew you were a player and a fake pastor! You’ve just prayed for all
your girlfriends, you think I didn’t hear you! Who the hell are Mercy,
Joy and Grace???”

Thursday, May 31, 2012

Watch your thoughts; they become words. Watch your words; they become actions. Watch your actions; they become habits. Watch your habits; they become character. Watch your character; it becomes your destiny. ~ Unknown

Friday, May 25, 2012

SEXUALITY, AIDS AND RELIGION: TRANSNATIONAL DYNAMICS IN AFRICA

Friday, May 18, 2012

english ni noma wakati mwingine

Mshikaji mmoja alikuwa na dingi yake, akamwona demu wake anakuja, bahati mbaya dingi alikua mkali sana, ili kuua soo, mazungumzo yao yalikuwa kama hivi:

MSHIKAJI: Umekuja kuchukua kile kitabu cha, speak English, my father doesn't know?

DEMU: Yeah! Na kile cha where should I wait 4 u?

MSHIKAJI: Dah! Hicho hakipo, labda kile cha wait 4 me under the coconut tree

DEMU: Sawa, ila usisahau na kile cha I am giving u 10 minutes

MSHIKAJI: Yeah, nita...ta...kupa na kile cha I won't let u down

DINGI: Mbona vingi sana, atavisoma kweli?

MSHIKAJI: Aahh! Huyu anasoma sana vitabu na ndio anatuongoza darasani.

DINGI: Mpe basi na kile cha I am not that much stupid na kile cha I have understood everything u spoke

Thursday, May 17, 2012

nimepata ujumbe huu kuhusu dini

"KAKA

dini ni ujinga na ni ulevi usio kuwa na mantiki epukeni Dini ila Dini zetu ziwe ni upendo"


Wednesday, May 16, 2012

tucheke kanisani

kuna mchungaji mmoja katika mahubiri yake huwa anachangamsha sana waumini wake,kwa mfano utakuta katikati ya mahubiri utasikia "..Muambie jirani yako..Yesu anakupenda!" basi kwa furaha na mbwembwe kila mtu atamuambia
  jirani yake,kisha mchungaji anasema "pokea upendo wa bwanaa!"..Sasa siku hiyo mchungaji alikuwa anahubiri kuhusu wanawake wasiopata watoto,sasa katikati ya mahubiri akasema "...Muambie jirani yako,mwaka huu utapata
  mimba!" bila kujali watu wamekaa na nani jirani wengi walikaa kimya kwani unakuta wengine walikuwa wamepakana wanaume tupu.Mara ikasikika tu mtu kapigwa kofi huko nyuma halafu mtoto akaanza kulia ile kunageuka wanakutana> na baba akimwambia mwanae wa kiume "..
Ukome!".Watu wote kanisani mbavu ziligongana kwa kicheko.

Tuesday, May 15, 2012

Yusufu wa Alimatiya ndiye baba wa kibaiolojia wa yesu???

nisihukumiwe ni habari ya kusikia hii


 nilisikia yakuwa yule Yusuf wa Almatiya (sio seremala), ndie aliyempachika mimba bikra maria. Yusufu alikuwa mzee wa heshima huko uyahudi na alikuwa msomi na cheo serikalini. tamaa ilimshinda akampachika mimba binti mdogo mariam. kumbuka adhabu ya kosa kama hilo ilikuwa ni kupigwa mawe mpaka mauti. basi ikabidi wazee wenye busara (malaika) wakae na kutafuta jinsi ya kumnusuru mwenzao katika hili, wakakaa na kugundua kuwa alikuwa akitarajiwa kuzaliwa Messiah, basi wakasema hapa ndo penyewe, tuseme hii ni mimba ya roho mtakatifu, imeingia kwa njia ya roho mtakatifu. Yusuphu seremala alikuja juu kwani mchumba wake ana mimba na hajawahi kulalanaye, wakamwonya akae kimya maana hii ni mimba ya kubwa.

akachaguliwa mzee (malaika) Gabriel kwenda kumpa habari Mariam, akamwambia 'usiogope' kwa nini hasiogope?? hamna kifo cha kupigwa mawe tena!


basi kama unajua kanuni za nguvu, maria kaaminishwa hivyo na jamii ikaaminishwa hivyo ikapeleka nguvu huko. yesu mwenyewe aliaminishwa na kupata nguvu hizo nk

wanasema yesu alikulia vyuoni huko alikokuwa akifundisha yosefu, baadae akahamia kwa wabuddha na kurudi kwao kupiga injili. na wanasema ndio maana Yusufu wa alimatiya alikuja kuchukua mwili wa yesu na kuuzika!


Monday, May 14, 2012

niliwahi kutoa maoni haya juu ya uafrika

tunapojadili masuala kama haya inabidi tuwe makini sana badala ya kujilaumu na kujiona wajinga, tuangalie uhalisia wa mambo. mimi sio msomi kama nyie na sijaenda ulaya japo sipatamani sana lakini tusiungane na wazungu kujionyesha kwamba hatuwezi lolote. kuna sehemu nimesoma kwamba chuo kikuu cha kwnza kilikuwa misri na mpaka sasa kuna vitu vya ajabu kwenye library za nchini mali. kijijini kwentu yamegundulika maandiko ya zaidi ya miaka 2000 kwenye miamba. inabidi mjue jinsi wakoloni walivyokata mikono na kuwauwa wanasayansi wetu aka wachonga vyuma.

kule kwetu BKB kuna nguo za mabaka ya miti, viatu vya miti na migomba na kuna nyumba nzuri za asili. vibuyu vizuri vya kunyweo pombe maji nk na kuna nyumba zilizojengwa kwa nyansi, udongo, miti nk.

pia tuna mitumbwi ya miti, pombe ya ndizi (lubisi) nk.

haya na mengine mengi hatukufundishwa na mzungu yeyote. hata hivyo mkumbuke kwamba tuliishi tangu dunia kuumbwa bila mzungu kuja africa wala nini na maisha yalikuwa mazuri na tulikula vyakula vya asili na kutumia madawa ya asili bila kuwa na side-effects. hata vifaa vyetu havikuwa na side effects na hatakuleta matatizo kama global warming.

mpaka sasa sisi bado tunaamini katika utu, umoja, undugu nk. ninyi milosoma na kwenda nje inabidi mjue kabisa kwamba mliyoyasoma na mnayoendelea kuyasoma ni mawazo, mitizamo nk vya wazungu ambao wanawajengea picha ya kujidharau ili muwatumikia bila swali!!

kaeni ulaya na US sisi tunaishi pia. kama waafrica hatutamani sana mali kwani tunajua mali zinaachwa lakini "utu" tunaondoka nao. tofauti yako wewe msomi na mzee wa Bugandika au bugabo ni kwamba wewe unaishi maisha ya wasiwasi na hofu wakati yule wa kijijini katulia na ana amani ya kutosha!

hata imani zetu ni nzuri ukilinganisha na za wazungu. soma makala ya padri kalugendo juu ya wamisionari wa ulaya na mungu wa watu weusi.

kauli zenu za kisomi kama hizi, zaweza kunifukuza mahali hapa kwenye blogu hii kama mtaendelea kuangalia uafrika wetu kwa mkabala wa kizungu tu kwamba nyie mnajua upande mmoja tu.

OKOKENI MUNGU WA WAISRAEL ANAKARIBIA KURUDI WAKATI WA WAAFRIKA YUPO NA HAKUWAHI KUONDOKA! ANATUPENDA!

Tuesday, May 8, 2012

Munga Tehenan, ni mwaka mwingine wa kifo chake

ni kweli, huyu bwana alikuwa wa aiana yake, mwaka 2007 alibadilisha maisha yangu kabisa na kunifanya nijitambue. namshukuru huyu bwana na kufurahia maisha kutokana na mafundisho yake. nashindwa kumlilia kutokana kifo chake kwani aliniaga kuwa ataondoka (kufa?) na kuniambia kuwa nisilie kwani kuondoka kwake ni furaha na sio mateso. alikomesha hisia za kulia na badala yake kufikiri

Munga Tehenan, sitomsahau milele huyu bwana. ni kweli jumamosi iliyopita, imetimia miaka 4 tangu huyu jamaa aondoke mwilini. alituaga tusimuelewe tulikuja kuelewa baada ya kuondoka kwake. hata hivyo, namshukuru japo hapendi shukuruni hizi kwa kunibadilisha kwani aliamini ni wajibu wake nakuwa nilijibadili mwenyewe na sio yeye. roho hii ya unyenyekevu, sitoisahau milele.

nitayaishi yoote aliyonifundisha na kuwagawia wengine